Psalms 52:1-6
Hukumu Ya Mungu
(Kwa Mwimbishaji: Utenzi Wa Daudi. Baada Ya Doegi, Mwedomu, Kumwendea Sauli Na Kumjulisha Kuwa Daudi Amekwenda Nyumbani Kwa Ahimeleki)
1 aEwe jitu, mbona unajivunia ubaya?
Kwa nini unajivuna mchana kutwa,
wewe ambaye ni fedheha mbele za Mungu?
2 bUlimi wako hupanga mashauri mabaya ya maangamizi.
Ni kama wembe mkali, ninyi mfanyao hila.
3 cUnapenda mabaya kuliko mema,
uongo kuliko kusema kweli.
4 dUnapenda kila neno lenye kudhuru,
ewe ulimi wenye hila!
5 eHakika Mungu atakushusha chini
kwa maangamizi ya milele:
atakunyakua na kukuondoa kwa nguvu
kutoka hema yako,
atakung’oa kutoka nchi ya walio hai.
6 fWenye haki wataona na kuogopa,
watamcheka, wakisema,
Copyright information for
SwhKC